Tangazo la Nafasi ya Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Singida 2025

 

Tangazo la Nafasi ya Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Singida 2025

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida amepokea kibali cha utekelezaji wa Ajira mpya katika mwaka wa fedha 2023/2024 na 2024/2025 kwa barua yenye Kumb. Na.FA.97/228/01/A/25 cha tarehe 26/04/2025 na barua yenye kumb Na. FA.97/288/01/09 ya tarehe 25/06/2024, kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.  

MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI.

➢ Waombaji wote wawe ni raia wa Tanzania wenye umri usiozidi miaka 45 na umri usiopungua miaka 18,

➢ Waombaji waambatanishe Cheti cha Kuzaliwa,Waombaji waambatanishe amelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye Anuani, Namba za Simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (Referees) wa kuaminika,

➢ Waombaji wote waweke nakala za vyeti vya taaluma na vyeti vya Kidato cha Nne na Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika kwenye Ajira Portal,

➢ Testimonials “Provision Results”, “Statement of Results” Hati ya Matokeo ya Kidato cha Nne na Sita HAVIKUBALIKI,

➢ Waombaji wote waweke picha mbili “Passport Size” ya hivi karibuni katika ukurasa wa Ajira Portal,

➢ Waombaji waliosoma nje ya nchi wahakikishe vyeti vyao vinahakikiwa na kuthibitishwa na mamlaka husika yaani TCU, NECTA na NACTE,

➢ Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi,

➢ Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa Umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka wenye Kumb. Na. CAC.45/257/01/D/140 wa tarehe 29 Novemba, 2010

➢ Uwasilishwaji taarifa na sifa za kughushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria,

➢ Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 10 Juni, 2025,

DOWNLOAD PDF YA TANGAZO


Next Post Previous Post